Skip to main content
Uwezo wa kusikia

Kufuta na kuosha masikio

Somo: 3 ya 5
Mada: 4 ya 5
 Imekamilika  kwa 0%

Kufuta na na kuosha masikio kUnaweza kuwa sehemu muhimu ya upimaji wa afya ya masikio.

Maelekezo

Jifunze kuhusu wakati gani unapaswa kufuta masikio, na wakati unapaswa kuosha masikio.

Kufuta masikio

Unapaswa kufuta masikio ya mgonjwa Ikiwa mtu huyu anatokwa uchafu.

Kufuta sikio ni njia salama ya kuondoa uchafu unaotoka kwenye sikio la mgonjwa.

Onyo

Usifute sikio la mgonjwa Ikiwa anapata maumivu makubwa unapofanya hivyo.

Elezea

Omba ruhusa kabla ya kufuta uchafu wa mgonjwa na mwelezee kile utakachofanya.

Nawa mikono yako

Osha mikono yako kila wakati kwa sabuni na kausha kabla na baada ya kufuta uchafu kwenye masikio.

Fanya maandalizi

Pinda sehemu ya mwisho ya kitambaa ambacho ni safi ili kutengeneza 'utambi wa tishu'.

A rolled up tissue with a flat end.

Kufuta uchafu unaotoka kwenye sikio

Shikilia utambi wa tishu kwa mkono wako wa kulia kama unachunguza sikio la kulia la mgonjwa , na mkono wako wa kushoto Ikiwa unachunguza sikio la kushoto la mgonjwa.

  1. Taratibu vuta pina kwa juu na nyuma kama unampima mtu mzima au kwa nyuma kama unampima mtoto
  2. Zungusha taratibu utambi wa tishu kwenye mfereji wa sikio la mgonjwa kwa sentimeta 2 hadi 3.
  3. Uache kwenye sikio kwa takriban sekunde 10
  4. Vuta utambi na uone kama una usaha au umajimaji mwingine juu yake
  5. Tupa utambi ambao umeutumia hivi punde. Fuata miongozo ya eneo ulipo kuhusu kutupa utambi uliotumika kwenye masikio
  6. Rudia zoezi kwa kutumia utambi mwingine wa tishu
  7. Endelea kurudia zoezi hadi utambi wa tishu usiwe na unyevunyevu wowote
  8. Angalia katika sikio la mgonjwa kwa kutumia otoskopu ili kuthibitisha kama uchafu wote umeondolewa.
Shikilia utambi wa tishu
Vuta pina kwa nyuma taratibu
Ingiza utambi wa tishu
Acha utambi wa tishu ndani ya sikio kwa takribani sekunde 10

Maelekezo

Tazama Video ya kufuta uchafu kwenye sikio la mgonjwa.

Kazi

Washiriki wakiwa kwenye jozi:

  1. Eleza kwamba, kwa idhini yao, utasafisha masikio yao ili kuondoa majimaji
  2. Fanya mazoezi ya kuandaa utambi wa tishu
  3. Ingiza utambi wa tishu ili kusafisha sikio la mgonjwa.

Una maoni gani kuhusu kusafisha sikio kwa kufuta uchafu?

Kuosha masikio

Kuosha sikio hutumiwa kusafisha nnta au kitu kutoka nje ya mwili kilicho kwenye mfereji wa sikio la mgonjwa.

Haupaswi kuosha sikio Ikiwa mfereji wa sikio wa mgonjwa bado haujazibwa na nnta ya sikio.

Onyo

Uoshaji sikio haufai kufanywa kama mgonjwa:

  • Amefanyiwa upasuaji wa sikio hivi karibuni
  • Ana tundu kwenye ngoma ya sikio
  • Maambukizi ya sikio
  • Maumivu ya sikio.

Ikiwa jibu ni ndio kwa swali lolote hapo juu, toa rufaa kwenda kuonana na mtaalamu wa huduma ya masikio na kusikia.

Seti /Mfuko wa vifaa vya kuosha masikio

Utahitaji:

  • Maji safi (yaliyochemshwa na kupozwa hadi kuwa sawia na joto la mwili)
  • Sindano ya mililita 20 (bila sindano)
  • Sahani yenye umbo la figo au bakuli lingine
  • Tishu
  • Karatasi ngumu au kitambaa (kitakachofunika sehemu ya juu ya bega la mgonjwa).

Ni muhimu maji yawe na joto la mwili (joto kidogo).

Pima joto la maji kwa kumwaga maji ndani ya kifundo cha mkono wako. Yanapaswa kuwa na joto kidogo sio kuwa ya moto au ya baridi.

Sindano iliyojaa maji safi. Sindano iko kwenye sahani lenye umbo la figo.

Onyo

Kila mara kagua joto la maji kabla ya kuosha sikio.

Kama mtu anapata kizunguzungu wakati wa akioshwa sikio, sitisha na kagua tena joto la maji.

Swali

Maji yanapaswa kuwa joto gani ili yafae kuosha sikio?

Chagua jibu moja.




Jibu sahihi ni Joto kidogo!

Kama maji ni moto au baridi, yanaweza kumfanya mgonjwa kuhisi kizunguzungu. Maji ya moto pia yanaweza kumuunguza.

Elezea

Kila mara omba ruhusa kabla ya kuosha masikio na ueleze kile utakachofanya.

Nawa mikono yako

Kila mara osha mikono yako kwa sabuni na uikaushe kabla na baada ya kuosha masikio.

Fanya maandalizi

  1. Kagua joto la maji
  2. Jaza sindano na maji
  3. Mwambie mtu huyo kushikilia sahani yenye umbo la figo au bakuli nyingine chini ya sikio lake na kuibana kwenye shingo yake
  4. Weka ncha ya sindano kwenye mfereji wa sikio wa mgonjwa
  5. Elekeza sindano ili ielekee juu ya mfereji wa sikio, na nyuma kidogo.

Dokezo

Ncha ya sindano imewekwa vizuri ndani ya mfereji wa sikio la mgonjwa.

Uelekep ni mbali na ngoma ya sikio la mgonjwa. Hii ni salama na humfanya mgonjwa ajisikie vizuri zaidi.

Kuosha sikio

  1. Bonyeza sindano kusukuma maji kwenye mfereji wa sikio la mgonjwa
  2. Maji yatamwagika ndani ya bakuli na yanaweza kuwa na nnta au kitu chochote kutoka nje ya mwili
  3. Kagua sikio la mgonjwa kwa mara nyingine kwa kutumia otoskopu
  4. Rudia kuosha hadi nta ya sikio iliyoziba au kitu kutoka nje ya mwili utolewe
  5. Kagua sikio la mgonjwa kila baada ya kuosha.

Ikiwa sikio la mgonjwa bado limezibwa na nnta baada ya majaribio matatu, muombe arudi siku inayofuata na rudia kuosha sikio.

Ikiwa nnta ya sikio haijaondolewa baada ya kuosha mara mbili, kwa ruhusa ya mgonjwa huyo, toa ruhusa kwenda kuonana na mtaalamu wa masikio na kusikia.

Onyo

Sitisha kuosha masikio Ikiwa mgonjwa huyo aTAPata maumivu ya sikio unapjaribu kuosha sikio!

Maelekezo

Tazama Video ya mtoa huduma akionyesha jinsi ya kuosha sikio la mgonjwa.

Swali

Ni mara ngapi unapaswa kurudia kuosha sikio?

Chagua jibu moja.




Jibu sahihi ni Mara tatu !

Rudia kuosha sikio hadi mara tatu.

Kazi

Washiriki wakiwa katika vikundi, wafanye mazoezi ya hatua za kuosha masikio:

1. Panga vizuri mfuko wenye vifaa vya kuosha sikio
2. Tayarisha maji na sindano
3. Kagua ndani ya sikio la mgonjwa kwa kutumia otoskopu
4. Weka sindano, sahani yenye umbo la figo na kitambaa.

Onyo

Usisukume maji kwenye sikio la mgonjwa Ikiwa halijaziba.

0%
Kufuta na kuosha masikio
Somo: 3 ya 5
Mada: 4 ya 5