Dalili za matatizo ya afya ya macho

Maendeleo ya usoMaji Mada:

Katika Upimaji wa hisia za kusikia na kuona, unaangalia tu nje ya jicho la mtu.

Dalili za matatizo ya afya ya macho

Dalili zinazoonyesha kuwa mtoto ana tatizo la afya ya macho ni pamoja na:

  • Kuwa na tongotongo au usaha kwenye ukope na/au kwenye kope
  • Kutokwa na maji au uchafu wa kunata kutoka kwa macho
  • Kuwa na rangi nyekundu isiyo ya kawaida kwenye sehemu nyeupe ya jicho
  • Pale ambapo sehemu ya jicho/macho yenye rangi haionekani vizuri au ina 'rangi ya maziwa'
  • Macho/macho hayatazami uelekeo mmoja.

Maelekezo

Soma orodha ya ishara zilizozoeleka zinazoonekana za tatizo la afya ya macho na uangalie picha zinazoendana.

Tongotongo au usaha kwenye ukope na kope

Kutokwa na maji au uchafu wa kunata kwenye macho

Sehemu nyeupe ya jicho kuwa na rangi nyekundu

Sehemu ya rangi ya jicho inaonekana kuwa so saf au ina 'rangi ya maziwa'

Macho hayatazami uelekeo mmoja kwa pamoja (jicho moja, au macho yote mawili yanaangalia kwa ndani au kwa nje)

Onyo

Kutambua matatizo ya afya ya macho mapema ni muhimu. Ikiwa hayatatibiwa, shida za kiafya za macho zinaweza kusababisha uharibifu wa kudumu kwa macho. Hii inaweza kusababisha upofu.