Ruka hadi kwa yaliyomo kuu
Maono

Vioo kuza na darubini ni nini?

Somo: la 1 kati ya masomo 6
Mada: 1 kati ya Mada 3
0% Imekamilika

Vioo kuza na darubini ni vifaa saidizi vya uoni wa chini ambavyo hufanya vitu vionekane vikubwa.

Wanaweza kuwasaidia watu wenye uoni hafifu kuona vitu, picha au uchapishaji ambao hawawezi kuona vinginevyo.

kioo kuza kinachowekwa chini kwenye mkono, ambayo ni lenzi ya mviringo yenye fremu na mpini, ikitumiwa kupanua maandishi.

Vikuzaji

Vioo kuza husaidia kwenye uoni wa karibu (kuona vitu vilivyo karibu).

Kioo kuza kinaweza kukusaidia kwenye kazi kama vile:

  • Kusoma au kuandika
  • Shughuli za kushona au ufundi
  • Kuangalia vitu vidogo, vile vyenye vitu vingi vingi.

Mwanamke, akitumia kikuzaji cha mkono kusoma lebo kwenye bidhaa.

Darubini

Darubini husaidia kuona mbali (kuona vitu vilivyo mbali).

Darubini inaweza kusaidia kwenye kazi kama vile:

  • Kuona ubao mweusi waziwazi
  • Kutafuta watu au vitu vilivyo mbali.

Mwanaume akitumia darubini ndogo ya mkono kumuona mtu katika umati wa watu.

Majadiliano

  • Je, unajua mtu yeyote anayetumia kioo kuza au darubini?
  • Ikiwa ndio, inawasaidiaje kufanya shughuli wanazotaka kufanya?